WENGER AELEZA KISA CHA UGOMVI WAKE NA MOURINHO, ATOA KAULI TATA
Kocha Arsene Wenger amesema wala hatajuta kutokana na kitendo chake cha kumsukuma Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho.
Wenger
alishikana na Mourinho wakati timu zao zilipokutana kwenye mechi ye
Premier League kwenye Uwanja wa Stamford Bridge na Arsenal ikalala kwa
mabao 2-0.
“Nini cha kujuta, wala sitafanya hivyo. Nilikuwa ninatoka upande mmoja kwenda mwingine.
“Nilipogeuka nikakuta mtu yuko mbele yangu kabisa kanizuia.
“Halafu hasemi lolote, sasa unafikiri nitafanya nini,” alisema Wenger.
Mwamuzi wa akiba alilazimika kuingia kati kuwatenganisha makocha hao wasifikie kuchapana makonde.
Category: uingereza
0 comments