Rekodi 7 tofauti alizoweka Cristiano Ronaldo baada ya kufunga hat trick dhidi ya Bilbao

Unknown | 8:58 AM | 0 comments


10649779_808787392518541_1971687263503280706_n
Mwanasoka bora wa dunia Cristiano Ronaldo jana usiku alifunga magoli matatu na kutimiza jumla ya magoli 17 katika michuano yote aliyoitumikia Real Madrid.Magoli hayo yalimfanya Ronaldo aweke rekodi kadhaa kwenye historia ya soka na rekodi hizo zipo kama ifuatavyo:

*3 – Hii ni Hat trick ya 3 ya Ronaldo katika La Liga msimu huu na amefanikiwa kufunga hat tricks hizo katika kipindi cha siku 15 tu.
*111 – Mchezo wa jana usiku ulikuwa wa 111 kwa Ronaldo kuitumikia timu yake ya taifa au klabu na katika mechi hiz zote amefunga zaidi ya goli moja.
*Cristiano amekuwa mchezaji wa pili kufunga hat tricks 3 katika mechi 7 za raundi ya kwanza ya La Liga – baada ya Mariano Martin kufanya hivyo msimu wa 1943-44.
*Cristiano ndio mchezaji wa kwanza kufunga magoli 13 au zaidi katika mechi 7 za kwanza Liga – tangu alipofanya hivyo Echevaria katika msimu wa 1943.
*50 – Cristiano Ronaldo mpaka sasa ameshatoa assists 50 kwa wachezaji wenzie wa Real Madrid.
*190 – Magoli matatu aliyofunga Cristiano Ronaldo jana dhidi ya Athletic Bilbao yalimfanya atimize jumla ya magoli 190 katika mechi 171 alizoichezea Real Madrid kwenye ligi.
*9 – Gareth Bale mpaka sasa amempa Cristiano Ronaldo assists nyingi kwenye La liga tangu mwanzo mwa msimu uliopita – amempata assists 9.

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments