ARGENTINA YACHAPA MTU 7-0

Unknown | 9:20 AM | 0 comments

.

Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi amefunga mabao mawili akitokea benchi dakika ya 65 na kuiwezesha Argentina kushinda 7-0 dhidi ya Bolivia Uwanja wa BBVA Compass








MSHAMBULIAJI Sergio Aguero amefunga mabao mawili na kuseti matatu Argentina ikiifumua Bolivia 7-0 usiku wa kuamkia leo katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa BBVA Compass mjini Houston.
Mwanasoka Bora wa Ulaya, Lionel Messi amefunga mabaio mawili licha ya kuingia dakika 65 akitokea benchi, huku Ezequiel Lavezze akifunga mawili pia na linguine Angel Correa. Lavezzi alifunga dakika ya sita na 41, Aguero dakika ya 34 na 59, Messi dakika ya 67 na 75, wakati Correa alishindilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Bolivia dakika ya 84.
Kikosi cha Argentina kilikuwa; Romero, Casco/Roncaglia dk77, Funes Mori, Rodriguez, Mas, Pereyra, Kranevitter, Lamela/Banega dk77, Lavezzi/Correa dk81, Aguero/Tevez dk80 na Gaitan/Messi dk65.
Bolivia; Daniel Vaca, Raldes, Zenteno, Hurtado, Smedberg-Dalence/Ramallo dk65, Danny Bejarano/Cabrera dk46, Melean/Lizio dk46, Cardozo/Eguino dk46, Arce/Chumacero dk46, Martins na Veizaga

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments