BABA WA SERGIO AGUERO ADAI MTOTO WAKE ANAPENDA KWENDA BARCELONA

Unknown | 10:35 AM | 0 comments


BABA mzazi wa Sergio Aguero ameweka wazi kuwa mshambuliaji huyo wa Manchester City anapenda kujiunga na Barcelona na  vyombo vya habari nchini Hispania vimeripoti kuwa wababe hao wa Katalunya wanajiandaa kuweka mezani ofa ya paundi milioni 31.
Barcelona wapo tayari kufikia paundi milioni 47 ili kuinasa saini ya nyota huyo wa kimataifa wa Argentina kama Man City watakataa ofa yao ya kwanza.
Lakini kocha mpya wa Barcelona, Luis Enrique ameripotiwa kuvutiwa zaidi na Aguero na yuko tayari kumwaga kitita kirefu cha fedha kama Man City watakataa., hii ni kutokana na mtandao wa michezo wa Hispania.
Passion: Sergio Aguero's father claims he would 'love' to go to Barcelona amid reports of a £31m bid
Keen: New Barcelona head coach Luis Enrique is an admirer of Aguero and is driving the Catalans' bid
 
 
Aguero mwenye miaka 25, ana uhusiano mzuri na nyota wa Barcelona, Lionel Messi na Enrique anaamini kuwa kuwaweka pamoja kunaweza kuisaidia klabu na Argentina kwa ujumla.
Mkataba wa Aguero utamalizika mwaka 2017, lakini klabu yake inaweza kumuuza zaidi ya paundi milioni 36 walizotumia kumsajili mwaka 2011.
Aguero alikuwa na msimu mzuri Etihad licha ya kuwa na majeruhi. Alifunga magoli 28 na kuwasaidia Man City kubeba kombe la ligi kuu na Capital One.

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments