CHEKA ADROO NA MUIRAN, MIYEYUSHO APIGWA K.O RAUNDI YA KWANZA NA MTHAILAND

Unknown | 12:06 PM | 0 comments


Bondia Fransic Cheka (kushoto) akichapana na Gavad Zohrehvand wa Iran wakati wa pambano lao la Kimataifa la kirafiki lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar es salaam jana usiku. Katika pambano hilo mabondia hao walitoka droo ya kufungana point.
Bondia Fransic Cheka (kushoto) akiliana 'timing' na Gavad Zohrehvand wa Iran wakati wa pambano lao.
Bondia Fransic Cheka kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Gavad Zohrehvand wa Iran wakati wa mpambano wao.
Bondia Sukkasem Kietyongyuth kutoka Thailand (kulia) akimkalisha bondia Fransic Miyeyusho, katika raundi ya kwanza ya pambano lao la raundi kumi na kumaliza pambano hilo kwa K,O.
Bondia Fransic Miyeyusho (kushoto) akijitutumua kuendelea kupigana na Bondia Sukkasem Kietyongyuth kutokaThailand. Katika pambano hilo Miyeyusho alipigwa raundi ya kwanza kwa K.O.
Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' (kushoto) akimwadhibu Mustafa Dotto wakati wa pambano lao la utangulizi lililofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba jana usiku jijini Dar es salaam. Katika pambano hilo King class alishinda kwa pointi.
Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' (kushoto) akiendelea kumwadhibu Mustafa Dotto.

credit: mafoto web

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments