MRISHO NGASA AMZUNGUMZIA HAMIS TAMBWE WA SIMBA ... HII HAPA KAULI YAKE
Kwa mara nyingine tena katika kipindi cha wiki mbili, winga
machachari wa klabu ya Yanga Mrisho Khalfan Ngassa amemsifia
mshambuliaji wa timu mahasimu Simba Mburundi Amiss Tambwe.
Akitumia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter Mrisho Ngassa
alimsifia Tambwe kwa kumuita mshambuliaji bora. Hatua hiyo ya Ngassa
ilikuja baada ya Tambwe kufunga mabao mawili katika mchezo wa jana dhidi
ya Ruvu Shooting uliopigwa uwanja wa taifa na Simba kutoka na ushindi
wa 3-2.
Category: tanzania
0 comments