TAARIFA NJEMA KWA MAN UNITED JUU YA VAN PERSIE
Unknown |
8:45 AM |
0
comments
Wakala
wa Robin van Persie amekanusha taarifa zilizo zagaa kuwa Van Persie
ameshakubaliana na klabu ya Fenerbahce lakini ameweka wazi kuwa,
mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi anarejea Carrington (uwanja
wa mazoezi wa Man United) kujiunga na kikosi cha United kuanza mazoezi
baada ya mapumziko ya mwishoni mwa ligi.Inaeleweka
kuwa, mpaka sasa hakuna dili lolote lililofanyika kati ya Manchester
United na klabu hiyo ya Uturuki na vyanzo vya karibu kutoka kwa Van
Persie vinasisitiza kwamba, mchezaji huyo anataka kuendelea kusalia Old
Trafford kwa muda wote uliobakia kwenye mkataba wake.
Mshambuliaji
huyo mwenye miaka 31 amepanga kukutana na kocha Louis van Gaal ili
kufanya mazungumzo kujua nafasi yake kwenye kikosi hicho.
Alipoulizwa
kwamba Van Prsie huenda akaondoka na anatafuta timu yenye uwezo wa
kulipa pauini milioni 12 kufidia mkataba wake wa miezi 12 iliobaki
kwenye mkataba wake, Kees Voss alisema: “Kama Robin angekuwa amepata
timu mpya tungeshaitangaza. Na kwasasa nipo Uholanzi”.
“Naweza sema kwamba Robin atajiunga na Manchester United kwa ajili ya mazoezi ya kwanza kwa ajili ya msimu ujao”.
Kilakitu
kitategemea kama United watamsajili mshambuliaji mwingine, mshambuliaji
wa Argentina na klabu ya Napoli Gonzalo Higuai na Edinson Cavan ambaye
ni mkali mwingine wa timu ya taifa ya Uruguay na klabu ya PSG ndio
miongoni mwa washambuliaji wanapewa nafasi kubwa ya kusajiliwa na
Mashetani Wekundu.
Kama
Van Persie atakuwa ni mshambuliaji chaguo la tatu, atalazimika kuikacha
timu hiyo kwasababu nataka kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara
kwenye kikosi cha kwanza ili aweze kupata nafasi ya kuitwa kwenye kikosi
cha Uholanzi kitakachoshiriki michuano ya Euro mwaka 2016.
United
tayari wako sokoni kutafuta mshambuliaji wa kuchukua nafasi iliyoachwa
na Radamel Falcao na wanaweza wakamuuza Javier Hernandez ‘Chicharito’ na
kumtoa kwa mkopo James Wilson.
Category: uingereza
0 comments