YANGA SC YAICHAPA STAND UNITED 3-0

Unknown | 8:55 PM | 0 comments

YANGA SC imeibwaga Stand United mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni hii Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.
Ushindi huo unaifanya Yanga SC itimize pointi 10 baada ya mechi tano na sasa inakabana na Azam FC na Mtibwa Sugar kileleni.
Yanga SC ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza kwa bao 1-0, lililofungwa na Genilson Santana Santos ‘Jaja’ dakika ya 13 baada ya kupokea pasi ya Mbrazil mwenzake, Andrey Coutinho.
Kipindi cha pili, mshambuliaji Jerry Tegete aliyetokea benchi aliifungia Yanga SC bao la pili dakika ya 78 baada ya kupata pasi ya Hussein Javu, aliyetokea benchi pia.
Tegete tena aliingia Yanga SC bao la tatu dakika ya 89 na baada ya mashabiki walimbeba juu kwa kuchangia ushindi huo.

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments