IVO MAPUNDA ‘OUT’ MECHI YA WATANI WA JADI!
HABARI mbaya kwa mashabiki wa
Simba sc ni kwamba kipa namba moja wa klabu hiyo, Ivo Philip Mapunda
amepata majeruhi itakayomuweka nje ya uwanja kwa wiki nne.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo,
Seleman Abdallah Matola ‘Veron’ amesema kuwa Ivo ameumia kidole chake
leo katika mazoezi ya klabu hiyo visiwani Zanzibar na daktari wa timu
amethibitisha.
Mapunda ataikosa mechi ya watani wa jadi oktoba 12 mwaka huu uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Hata hivyo, Matola amesema
kukosekana kwa Ivo sio tatizo kubwa kwasababu wana makipa wengine kama
Hussein Sharif ‘Casillas’ na kipa Peter Manyika ambao wanaweza kufanya
kazi vizuri.
Casillas na Manyika walisajiliwa
majira ya kiangazi mwaka huu baada ya mnyama kuachana na kipa Mghana Yaw
Berko mwishoni mwa msimu uliopita na kubaki na Ivo.
Majeruhi wanazidi kuongezeka Simba ambapo mpaka sasa Jonas Mkude hayuko fiti kucheza kwa sasa ingawa ameshaanza mazoezi mepesi.
Mkenya Pual Kiongera naye aliumia
mechi ya jumapili iliyopita dhidi ya Coastal Union na taarifa
zilizotoka jana ni kwamba ana majeruhi sugu ya goti.
Ilifahamika kuwa Kiongera naye atakaa nje ya uwanja kwa wiki sita au miezi miwili.
Naye beki wa kushoto Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ anasumbuliwa na majeruhi na hana uhakika wa kucheza mechi ijayo.
Simba imejificha Zanzibar
kujiandaa na mechi ijayo ya ligi kuu dhidi ya Polisi Morogoro itayopigwa
jumamosi (septemba 27 mwaka huu) uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Category: tanzania
0 comments