Home �
uingereza
� BRAZIL YAANZA KWA KUITANDIKA CROATIA 3-1, NEYMAR APIGA MAWILI NA KUKIMBIA KADI NYEKUNDU...OSCAR NAYE APIGA MPIRA MKUBWA MNO
Unknown |
8:50 AM |
0
comments

Neymar Mkombozi: Mbrazil huyo anayevaa jezi namba 10 alifunga mawili.
NYOTA aliyebeba matumaini ya
Wabrazil wengi, Neymar amefunga mabao mawili usiku huu katika ushindi wa
mabao 3-1 dhidi ya Croatia kwenye mchezo wa ufunguzi wa fainali za
kombe la dunia.
Wenyeji walijifunga mapema dakika
ya 7 ya kipindi cha kwanza baada ya Marcelo kuujaza mpira nyavuni katika
harakati za kuokoa na kuzua ukimya mkubwa uwanjani kwa mashabiki wa
Brazil waliofurika kushuhudia timu yao..
Mambo almanusura yawe mabaya kwa
Brazil wakati Neymar alipomfanyia faulo mbaya kiungo wa Croatia Luka
Modric, lakini mwamuzi Yuichi Nishimura alimzawadia kadi ya njano tu.
Baadaye Neymar alifunga bao la
kusawazisha kwa shuti la mbali na aliongeza bao la pili kwa njia ya
mkwaju ya penati baada ya mwamuzi kutoa penati yenye utata kufuatia
Dehan Lovren kumfanyia madhambi Fred.
Oscar alihitimisha karamu ya mabao
kwa Wabrazil na kutoka na ushindi wa kwanza katika michuano ya mwaka
huu inayofanyika katika ardhi yao.

Mkwaju wa penati: Neymar alifunga penati yake ingawa kipa wa Croatia aligusa mpira.
You might also like:
Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Category:
uingereza
0 comments