DIEGO COSTA AUMIA VIBAYA AKIIFUNGIA BAO LA PILI ATLETICO JANA, SASA HATARINI KUIKOSA CHELSEA LIGI YA MABINGWA
MSHAMBULIAJI
Diego Costa anakabiliwa na mtihani wa kupambana na muda ili kuwa fiti
kabla Atlético Madrid haijakutana na Chelsea katika Nusu Fainali ya Ligi
ya Mabingwa Ulaya, baada ya kuumia ugoko wakiifunga Getafe 2-0 jana.
Mshambuliaji
huyo wa Hispania alitolewa nje baada ya kujigonga kwenye nguzo ya goli
wakati akiifungia timu hiyo bao la pili katika La Liga.
Costa
anaweza kukosa mechi dhidi ya The Blues zitakapokutana nchini Hispania
Aprili 22, mwaka huu. Ushindi wa jana unaifanya Atletico ijisogeze
jirani kabisa a ubingwa kwa kufikisha pointi 82 baada ya kucheza mechi
33, ikifuatiwa na Real Madrid yenye pointi 79 za mechi na Barcelona
pointi 78 za mechi 33 pia.
Diego Costa alivyogonga nguzo wakati anafunga
Costa anapiga shuti ugoko unakwenda kugonga nguzo ya goli
Costa akiugulia maumivu
Costa anatolewa nje kwa machela
Category: uingereza
0 comments