Barcelona yamsajili golikipa mpya kumrithi Valdes
Klabu
ya FC Barcelona imetangaza kufikia makubaliano na Borussia
Monchengladbach juu ya uhamisho wa golikipa Marc-Andre ter Stegen kwa
ada inayokaribia kiasi cha €9-12 million pamoja na kucheza mechi mbili
za kirafiki, gazeti la kihispania la Marca limethibitisha.Barca walikuwa
sokoni kwa muda mrefu wakijaribu kutafuta golikipa baada ya Victor
Valdes kutangaza angeondoka kwenye klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu na
sasa wamempata mrithi wake Ter Stegen.Golikipa huyu raia wa Ujerumani
atasaini mkataba utakaomuweka Barcelona mpaka 2019.
Category: uingereza
0 comments