JOHN TERRY AIOKOA CHELSEA ENGLAND

Unknown | 8:23 PM | 0 comments




BAO la dakika ya mwisho kabisa la Nahodha aliyerejea John Terry limeipa Chelsea ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Everton jioni hii katika Ligi Kuu ya England.

Ilikuwa kama Jose Mourinho tayari amekwishapoteza pointi mbili katika mbio za ubingwa kutokana na timu hizo kuwa hazijafungana hadi Phil Jagielka alipomchezea rafu Ramires.

Frank Lampard akaenda kupiga mpira wa adhabu  ambao uliguswa na Branislav Ivanovic na Terry akateleza kwenda kuusukumia nyavuni dhidi ya kipa Tim Howard.

Baada ya ushindi huo wa mbinde unaoifanya Chelsea itimize pointi 60 baada ya mechi 27 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu, na The Blues watasafiri hadi Galatasaray kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Hatua ya 16 Bora Jumatano.



Double act: Frank Lampard (left) and John Terry combined for Chelsea's crucial winner

Mkombozi: Frank Lampard (kushoto) na John Terry ushirikiano wao umeipa bao la ushindi ChelseaQuick off the mark: John Terry reacts first as Slyvain Distin, Leighton Baines and Phil Jagielka can only watch





John Terry alikuwa wa kwanza kuugusa mpira huku Slyvain Distin, Leighton Baines na Phil Jagielka wakiangaliaThe late show: John Terry slides in front of Tim Howard as Chelsea seal a dramatic late win



John Terry akiteleza kufunga dhidi ya Tim Howard 

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments