JOHN TERRY AIOKOA CHELSEA ENGLAND
BAO
la dakika ya mwisho kabisa la Nahodha aliyerejea John Terry limeipa
Chelsea ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Everton jioni hii katika Ligi Kuu ya
England.
Ilikuwa
kama Jose Mourinho tayari amekwishapoteza pointi mbili katika mbio za
ubingwa kutokana na timu hizo kuwa hazijafungana hadi Phil Jagielka
alipomchezea rafu Ramires.
Frank
Lampard akaenda kupiga mpira wa adhabu ambao uliguswa na Branislav
Ivanovic na Terry akateleza kwenda kuusukumia nyavuni dhidi ya kipa Tim
Howard.
Baada
ya ushindi huo wa mbinde unaoifanya Chelsea itimize pointi 60 baada ya
mechi 27 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu, na The Blues watasafiri hadi
Galatasaray kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Hatua ya 16 Bora
Jumatano.
Mkombozi: Frank Lampard (kushoto) na John Terry ushirikiano wao umeipa bao la ushindi Chelsea
John Terry alikuwa wa kwanza kuugusa mpira huku Slyvain Distin, Leighton Baines na Phil Jagielka wakiangalia
John Terry akiteleza kufunga dhidi ya Tim Howard
Category: uingereza
0 comments