KOMBE LA MAPINDUZI: KOCHA WA ITALIA PRANDELLI MGENI RASMI SIMBA VS AFC LEOPARDS
Na Baraka Mpenja, Dar es 
salaam
MAANDALIZI ya kombe la 
Mapinduzi linalotarajia kuanza kutimua vumbi januari mosi mwakani yanakwenda 
vizuri na timu zote zilizothibitisha kushiriki zinatarajia kuwasili desemba 31 
mwaka huu.
Msemaji wa kamati ya 
mashindano , Farouk Karim amesema kuwa timu za Tusker fc, AFC Leopard za Kenya, 
KCC, URA za Uganda , Simba sc, Yanga, Azam fc na Mbeya City za Tanzania bara 
tayari zimeshathibitisha kushiriki na kamati ya maandalizi imeshakamilisha  
taratibu za kuzipokea.
SIMBA imepangwa kufungua pazia la michuano ya Kombe la 
Mapinduzi kwa kucheza na AFC Leopards ya Kenya Januari Mosi wakati Yanga 
wakishuka dimbani siku inayofuata kuikabili Tusker FC.
Karim amesema mgeni 
rasmi katika mechi ya ufunguzi itakayopigwa januari mosi majira ya saa mbili 
usiku katika uwanja wa Aman kisiwani Unguja baina ya Simba sc dhidi ya AFC 
Leopard ya Kenya atakuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Italia,  Cesare 
Prandelli.
Pambano la Simba na Leopards litatanguliwa na mechi 
kati ya wenyeji KMKM na KCC ya Uganda litakalopigwa saa 10 jioni kwenye uwanja 
huohuo.
“Ninavyozungumza na wewe 
muda huu, Prandelli yupo hapa Zanzibar mapumzikoni na tayari amekubali kufungua 
michuano hii yenye maana kubwa katika miaka 50 ya mapinduzi ya Zanzibar”. 
Alisema Karim.
Karim alisema katika 
michuano ya mwaka huu viwanja viwili vitatumika ambavyo ni Gombani kisiwani 
Pemba na Aman Kisiwani Unguja.
“Uwanja wa Gombani upo 
katika hali nzuri na unavyojua una nyasi za bandia. Uwanja wa Aman umefanyiwa 
ukarabati mkubwa na hivi sasa wataalamu kutoka China wapo hatua za mwisho kabisa 
kukamilisha shughuli yao”. Alisema Karim.
Mratibu huyo alitoa wito 
kwa wadau, wapenzi wa soka visiwani Zanzibar kujitokeza kwa wingi kwani kamati 
ya mashindano inategemea mapato ya milangoni kufanikisha 
mipango.
“Michuano hii inagharimu 
zaidi ya shilingi milioni 600, hatuna fedha hizo, tunategemea mapato ya 
milangoni, hivyo mashabiki kufika kwao  kwa wingi ndio mafanikio yetu”. Aliomba 
Karim.
Aidha ameziomba taasisi 
na makampuni ya bara na visiwani kujitokeza kufanya matangazo katika michuano 
hiyo ili angalau wapate pesa za kuendeshea michuano 
hiyo.
Michuano iliyopita, Azam 
fc walitwaa ubingwa, lakini mwaka huu kuna changamoto mpya hasa kutokana na 
uwepo wa timu za Dar Young Africans na Mbeya City ambazo 
hazikushiriki.
Mechi zote za hatua ya makundi na robo fainali 
zitafanyika kwenye viwanja wa Gombani Pemba na Aman Unguja, wakati nusu fainali 
na fainali zitapigwa kwenye Uwanja wa Amani.
Katika michuano 
iliyopita Simba waliishia nusu fainali baada ya kuondolewa na Azam FC kwa 
mikwaju ya penalti 5-4 baada ya mechi kumalizika kwa sare ya 2-2 hata baada ya 
kuongezwa dakika 30.
Category: tanzania



0 comments