SIMBA YATOKA SARE YA 2-2 NYUMBANI NA WATOTO WA MBEYA CITY

Unknown | 10:11 PM | 0 comments

 


Timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, leo imecheshwa kwata na Vijana wa Mbeya city na kuvtwa shati katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliochezwa kwenye Uwanja wa taifa. 

Katika mchezo huo timu hizo zimetoka sare ya mabao 2-2, ambapo mchezaji wa Simba, Amis Tambwe mbaye wiki hii alinukuliwa na baadhi ya magazeti akijinadi kuwa mfungaji bora wa msimu huu, ameweza kuifungia timu yake mabao yote mawili katika dakika za 29 na 33.

Nao Mbeya City, timu ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya inayofundishwa na Juma Mwambusi, bao la kipindi cha kwanza lilifungwa na Paul Nonga dakika ya 37, wakati la kusawazisha lilifungwa na Richard Peter dakika ya 69.

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments