RATIBA YA ROBO FAINALI YA LIGI MABINGWA ULAYA HII HAPA

Unknown | 8:44 AM | 0 comments

uefa
Shirikisho la soka barani Ulaya UEFA, hivi punde limetoa ratiba ya mechi za Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya ambayo inaingia katika hatua ya robo fainali.
Zoezi hilo limefanyika katika ukumbi wa mikutano wa shirikisho la soka barani Ulaya UEFA uliopo mjini Nyon nchini Uswizi, kwa kuwashirikisha maofisa wa klabu zote nane ambazo zilifanikiwa kupenya katika hatua ya 16 bora.
Michezo ya hatua ya robo fainali imepangwa kuchezwa Aprili 5 na 6 na marudio ni Aprili 12 na 13.
Ratiba yenyewe ipo kama ifuatavyo:
Barcelona Vs Atletico Madrid
Bayern Munich Vs Benfica
Paris Saint Germain Vs Manchester City
Wolfsburg Vs Real Madrid

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments