RATIBA MPYA YA LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA HII HAPA YATOKA ...

Unknown | 9:14 PM | 0 comments


RATIBA MPYA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA;
Machi 16, 2016
Azam FC Vs Stand United
Machi 18, 2016
Kagera Sugar Vs Mtibwa Sugar
Machi 19, 2016
Coastal Union Vs Simba SC
Majimaji Vs Mbeya City
Stand United Vs Ndanda FC
Machi 20, 2016
African Sports Vs Prisons
Machi 21, 2016
Mgambo JKT Vs Toto Africans
Machi 24, 2016
African Sports Vs Toto Africans
Aprili 2, 2016
Majimaji Vs Simba SC
Yanga SC Vs Kagera Sugar
Toto Africans Vs Azam FC
Stand United Vs Mgambo JKT
Ndanda FC Vs Prisons
Mbeya City Vs Coastal Union
Aprili 3, 2016
JKT Ruvu Vs African Sports
Mwadui FC Vs Mtibwa Sugar
Aprili 5, 2016
Toto Africans Vs Yanga SC
Azam FC Vs Ndanda FC
Aprili 9, 2016
Stand United Vs Yanga SC
Ndanda FC Vs Mwadui FC

Na Somoe Ng’itu, DAR ES SALAAMSALAAM BIN ZUBERY
YANGA haitacheza mechi yoyote ya Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara mwezi huu, wakati wapinzani wao katika mbio za ubingwa, Simba na Azam watacheza mechi moja moja.
Kwa mujibu wa marekebisho ya Ratiba ya Ligi Kuu yaliyotolewa leo, Azam FC watacheza na Stand United kesho Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, wakati Simba SC watacheza na Coastal Union Jumamosi Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. 
Bodi ya Ligi imelazimika kufanya marekebisho ya Ratiba ya Ligi Kuu kupisha ratiba ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars katika mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika 2017.
Taifa Stars itakuwa na mchezo wa kufuzu AFCON Kundi G dhidi ya Chad mjini N’jamena Machi 25, kabla ya timu hizo kurudiana Machi 28, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Na baada ya mechi za mwishoni mwa wiki za michuano ya klabu barani, Afrika wachezaji wa Stars wanatarajiwa kukusanywa Jumapili kabla ya safari Jumanne kuelekea Chad.
Yanga SC baada ya ushindi wa 2-1 kwenye mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya APR Jumamosi mjini Kigali, watarudiana na timu hiyo ya jeshi la Rwanda Jumamosi wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Na Azam FC baada ya kushinda 3-0 mjini Johannesburg, Afrika Kusini dhidi ya wenyeji Bidvest Wits katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Kombe la Shirikisho Afrika, watarudiana na timu hiyo Jumapili, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Ligi Kuu itaendelea Aprili 2, kwa Yanga kumenyana na Kagera Sugar Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Simba SC kumenyana na Majimaji Uwanja wa Majimaji mjini Songea, wakati Azam FC watakuwa wageni wa Toto Africans Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments