BARCELONA YAIADHIBU ARSENAL BILA YA HURUMA

Unknown | 2:37 AM | 0 comments

Mshambuliaji wa Barcelona, Luis Suarez akiunganisha kwa ustadi mkubwa krosi ya Dani Alves kuifungia timu yake bao la pili dakika ya 65 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Arsenal usiku huu Uwanja wa Camp Nou katika mchezo wa marudiano wa hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mabao mengine ya Barcelona yamefungwa na Neymar Junior dakika ya 18 na Lionel Messi dakika ya 88, wakati bao pekee la Arsenal limefungwa na Mohamed Elneny dakika ya 51. Barcelona inatinga Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa 5-1 baada ya awali kushinda 2-0 Uwanja wa Emirates, London PICHA ZAIDI GONGA HAPA

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments