VAN GAAL AMTEMA ROONEY, AWABEBA HAWA SAFARI YA DENMARK MECHI YA EUROPA LEAGUE

Unknown | 7:52 PM | 0 comments


Morgan Schneiderlin (kulia) na Anthony Martial pichani wakiwa Uwanja wa Ndege wakati wa safari yao leo PICHA ZAIDI GONGA HAPA

KIKOSI CHA MAN UTD KINACHOKWENDA KUIVAA MIDTJYLLAND

David De Gea, Sergio Romero, Donald Love, Paddy McNair, Chris Smalling, Daley Blind, Regan Poole, Joe Riley, Michael Carrick, Ander Herrera, Morgan Schneiderlin, Jesse Lingard, Andreas Pereira, James Weir, Juan Mata, Memphis Depay, Anthony Martial na Will Keane.
NAHODHA wa Manchester United, Wayne Rooney ameondolewa kwenye kikosi cha wachezaji 18 kinachokwenda kumenyana na FC Midtjylland ya Denmark katika michuano ya Europa League keshi.
Kiungo Marouane Fellaini amekuwa mchezaji mwingine mzoefu aliyeachwa kwenye safari hiyo pamoja na beki wa pembeni Matteo Darmian.
Kocha Louis van Gaal amebeba wachezaji chipukizi zaidi katika safari hiyo, wakiwemo Regan Poole, Joe Riley na James Weir ambaye anaweza kuchezea kikosi cha kwanza kwa mara ya kwanza. Credit: Bin zubery

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments