YANGA YAPEWA VIBONDE COMORO

Unknown | 10:24 PM | 0 comments

Mabingwa wa Tanzania Yanga wamepata bahati katika mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa baada ya kupangiwa vibonde Komorozine ya Comoro.
Kama Yanga itafanikiwa kuvuka dhidi ya vibonde hao itakuwa na kazi ngumu dhidi ya mabingwa wa Afrika, Al Ahly.

Shirikisho la Soka Afrika (Caf) limeipa Yanga ratiba hiyo ngumu ambayo ulahisi katika mechi ya kwanza na kigingi inayofuatia.
Kwa upande wa Zanzibar, mabingwa wake KMKM wamepangwa kuanza na wabishi Dedebit ya Ethiopia ambao miaka mitatu iliyopita waliing’oa Yanga iliyokuwa inanolewa na Sam Timbe.
Yanga       Vs Komorozine,
Februari 7-9, marudio Februari 14-16
Yanga ikipita inataivaa
Yanga       Vs Al-Ahly
Ferbuari 28-Machi 2, marudio Machi 7-9

Dedebit    Vs     KMKM
Februari 7-9 Feb, marudio Februari 14-16

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments