YANGA YAPEWA VIBONDE COMORO
Mabingwa wa
Tanzania Yanga wamepata bahati katika mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa baada
ya kupangiwa vibonde Komorozine ya Comoro.
Kama Yanga
itafanikiwa kuvuka dhidi ya vibonde hao itakuwa na kazi ngumu dhidi ya mabingwa
wa Afrika, Al Ahly.
Shirikisho la
Soka Afrika (Caf) limeipa Yanga ratiba hiyo ngumu ambayo ulahisi katika mechi
ya kwanza na kigingi inayofuatia.
Kwa upande wa
Zanzibar, mabingwa wake KMKM wamepangwa kuanza na wabishi Dedebit ya Ethiopia
ambao miaka mitatu iliyopita waliing’oa Yanga iliyokuwa inanolewa na Sam Timbe.
Yanga Vs
Komorozine,
Februari 7-9,
marudio Februari 14-16
Yanga ikipita
inataivaa
Yanga Vs Al-Ahly
Ferbuari 28-Machi
2, marudio Machi 7-9
Dedebit Vs KMKM
Februari 7-9
Feb, marudio Februari 14-16
Category: tanzania
0 comments