MAN U WAKUBALI KICHAPO

Unknown | 10:44 PM | 0 comments

MAMBO yamezidi kumuendea kombo kocha David Moyes Manchester United, baada ya leo pia kufungwa 1-0 na Newcastle United bao pekee la Yohan Cabaye dakika ya 61.
Ushindi umemaliza kiu ya ushindi ya Newcastle ya miaka 41 Uwanja wa Old Trafford.
Kipigo hicho cha pili mfululizo nyumbani katika Ligi Kuu, ambayo ni mara ya kwanza tangu mwaka 2002, kinaamisha msimu huu tayari United imefungwa mechi tano na wameambulia pointi mbili tu katika mechi zao nne zilizopita.
Kisu cha mgongo: Yohan Cabaye akishangilia bao lake pekee lililoizamisha Man United leo
No you don't: David Moyes keeps the ball away from Hatem Ben Arfa on the sidelines
Haiwezekani: David Moyes akiukwepesha mpira ili Hatem Ben Arfa asiuchukue

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments