MAN UNITED YAUA 3-1 NA KUFUZU EUROPA LEAGUE

Unknown | 7:44 PM | 0 comments

TIMU ya Manchester United imefanikiwa kukata tiketi ya kucheza michuano ya Europa League baada ya ushindi wa mabao 3-1 usiku huu dhidi ya Bournemouth katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Old Trafford leo, ilikuwa ufanyike juzi lakini ukaahirishwa kutokana na hofu kutegwa kwenye Uwanja huo. 
Nahodha Wayne Rooney aliifungia United bao la kwanza akimalizia krosi ya Anthony Martial dakika ya , hilo likiwa bao lake la 100 kufunga Uwanja wa Old Trafford.

Nahodha wa Man United, Wayne Rooney akipongezwa na wachezaji wenzake baada ya kuiwezesha timu yao kufuzu Europa League kwa kumaliza nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England PICHA ZAIDI GONGA HAPA

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments