MESSI AUWASHA MOTO MPYAA BARCELONA

Unknown | 9:07 AM | 0 comments


MSHAMBULIAJI Lionel Messi amewasha moto Barcelona baada ya kumuambia Mkurugenzi wake hajui lolote kuhusu soka.
Maelezo hayo ni majibu kwa Javier Faus ambaye wiki mbili zilizopita alisema kwamba Barcelona haina sababu ya kuketi chini na mwanasoka huyo kujadili Mkataba wake wa sasa. 
Amejibu: Lionel Messi amesema Mkurugenzi wa Barcelona, Javier Faus hajui lolote kuhusu soka baada ya kusema hakuna haja ya kujadili Mkataba wa sasa wa Muargentina huyo
Lionel Messi
Akizungumza na Redio ya Catalan, RAC1 kutoka Argentina, Messi alisema: "Barcelona ni klabu bora duniani, inawakilishwa na wajumbe bora wa bodi pia. Senor [Javier] Faus ni mtu ambaye hajui lolote kuhusu soka na anataka kuongoza Barcelona kama biashara, ambayo siyo,".
Alisema: "Mbali na hayo, ningemkumbusha kwamba hata hakuna mtu yeyote kutoka kambi yangu ameulizia kuhusu ongezeko lolote la mshahara na anafahamu hilo,".
Golden boy: Messi is Barca's prize asset and won the European Golden Boot for 2013
Mwana wa dhahabu: Messi ni bidhaa adimu ndani ya Barca na ndiye mahinsi wa Kiatu cha Dhahabu Ulaya mwaka 2013

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments