MAJANGA MAN U

Unknown | 10:57 PM | 0 comments

BEKI Patrice Evra amesema kwamba ataondoka Manchester United mwishoni mwa msimu.
Beki huyo wa kushoto wa Ufaransa aliulizwa kuhusu Mkataba wake ambao unamalizika Juni na kama ataongeza na majibu yake yalikuwa anataka kuondoka Old Trafford.
Evra ameumizwa na kuondoka kwa Sir Alex Ferguson aliyestaafu na hajapendezewa na mpango wa klabu hiyo kutaka kuwasajili Leighton Baines na Fabio Coentrao.

Anabaki au anaondoka? Patrice Evra inasemekana anataka kuondoka Manchester United
Staying or going? Patrice Evra seems destined to leave Manchester United
Alisema: "Hapana, hapana kabisa. Ni mambo binafsi. Si kwamba Manchester United haitaki mimi nisaini mkataba mpya. Hii kwa ujumla na mambo binafsi. Manchester United wandependa mimi nimalizie soka yangu huko, lakini hiki ni kitu fulani binafsi,".
Mtendaji Mkuu wa United, Ed Woodward amewaambia mashabiki kwamba Baines alikuwa mlegwa wa awali wa klabu, lakini Everton ilitaka dau kubwa kumuuza.
Evra amekuwa akihusishwa na mpango wa kurejea kwao Ufaransa kujiunga na klabu yake ya zamani, Monaco na matajiri wa nchini humo, Paris Saint-Germain kwa miezi kadhaa.
Target: Manchester United wanted to bring in Leighton Baines who may have displaced Evra
Mlengwa: Manchester United walitaka kumsajili Leighton Baines ambaye anaweza kumpindua Evra kikosi cha kwanza
Blow: Evra was also sad that legendary manager Sir Alex Ferguson left the club
Pigo: Evra pia hakufurahishwa na kuondoka kwa kocha gwiji wa klabu hiyo, Sir Alex Ferguson

Evra pia anakabiliwa na moto mwingine kutokana na kuwashambulia kwa maneno wachambuzi wa soka wa nchini mwake. 
Ametakiwa na Shirikisho la Soka Ufaransa kufafanua madai yake, ambayo yamemhusisha pia mshindi wa Kombe la Dunia mwaka 1998, Bixente Lizarazu na wachambuzi wengine watatu kwenye TV.

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments