KUELEKEA BRAZIL 2014: HATIMA YA UFARANSA, HISPANIA, ENGLAND KUJULIKANA LEO

Unknown | 11:29 AM | 0 comments



LONDON, England 



Tayari makundi ya A, B, C, D, na E yalishapata vinara watakaoiwakilisha Ulaya nchini Brazil, ambapo nchi za Ubelgiji, Italia, Ujerumani, Uholanzi na Uswisi zimefuzu fainali hizo, huku makundi ya F, G, H na I yakitarajia kupata vinara wake leo


KINYANG’ANYIRO cha kuwania tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil, Kanda ya Ulaya kinaendelea leo kwa miamba minne kusakwa kukamilisha idadi ya timu za bara hizo, baada ya nyingine tano kujikatia tiketi zake.


Tayari makundi ya A, B, C, D, na E yalishapata vinara watakaoiwakilisha Ulaya nchini Brazil, ambapo nchi za Ubelgiji, Italia, Ujerumani, Uholanzi na Uswisi zimefuzu fainali hizo, huku makundi ya F, G, H na I yakitarajia kupata vinara wake leo.


Shughuli pevu leo inayakabili mataifa ya Ufaransa, Hispania, England, Ugiriki, Ureno na Russia, zitakazoshuka kwenye viwanja mbalimbali kuwania pointi muhimu, huku nyingine zikiombea mabaya kwa wapinzani kuweza kujihakikishia tiketi ya Brazil.


Mabingwa watetezi, Hispania na kikosi kinachonolewa na Fabio Capello cha Russia, vitakuwa na kibarua kipevu cha kuzipiku Ufaransa na Ureno katika jaribio la kufuzu fainali za mwakani, ingawa miamba itakayozidiwa kete hapo itakuwa na mechi za mtoano wa ‘best-losers.’


Mechi za mtoano ‘best losers play-off’ utajumuiosha timu nane zenye matokeo bora kutoka katika makundi yote, ili kupata timu nne zitakaoungana na vinara tisa kufanya jumla ya timu 13 za bara la Ulaya zitakazofuzu Brazil 2014.


Hispania inaingia dimba la nyumbani kusaka sare dhidi ya Georgia ili kufuzu fainali za mwakani, bila kujali matokeo ya Ufaransa itakayokuwa nyumbani kuikaribisha Finland, kama ilivyo pia kwa Russia, inayohitaji pointi pia dhidi ya Azerbaijan kuitibulia Ureno.


Russia inaizidi Ureno pointi tatu, hivyo ukiondoa sare kuweza kufuzu Brazil, itahitaji maombi ili Ureno ipoteze nyumbani dhidi ya Luxemburgo, matokeo yatakayoiacha juu ya kilele cha kundi F la michuano hii ya awali.


Katika kundi H, England na Ukraine zote zina nafasi ya kufuzu fainali zijazo, ambapo ‘Three Lions’ wanaongoza kwa pointi 19, moja juu ya Ukraine, ambapo kila moja inaiombea mabaya yenzake huku ikihitaji ushindi kujihakikishia tiketi ya moja kwa moja.


England watakuwa nyumbani Wembley kuwaalika Poland ambao wanakamilisha ratiba, huku Ukraine wao wakiwa ugenini kuwavaa wenyeji wao San Marino – ambao wana rekodi chafu ya kufungwa mechi zote tisa za kundi hilo, ikiburuza mkia bila pointi.


Katika kundi la G, Bosnia-Herzegovina wanaongoza kwa tofauti ya mabao juu ya Ugiriki, kila moja ikiwa na pointi 22, hivyo mechi zao leo ni za kufa na kupona katika jaribio la kufuzu kwa fainali za mwakani.


Wakati vinara Bosnia-Herzegovina watakuwa ugenini kuwavaa Lithuania, wapinzani wao Ugiriki watakuwa nyumbani kuwaalika ‘vibonde’ Liechtenstein, ambao wanabuiruza mkia wa kundi G wakiwa na pointi mbili baada ya mechi zao tisa.


Jijini London, England wanaingia dimbani wakiwa na kumbukumbu ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Poland kwenye dimba la Wembley, iliyowanyima tiketi ya kufzu fainali za Kombe la Dunia la mwaka 1974.


Licha ya rekodi hiyo, kocha wa England, Roy Hodgson meonesha shaka ya kuwashinda Poland, hasa kutokana na ushindani na wakati mgumu waliowapa katika mechi ya kwanza baina ya nchi hizo iliyopigwa jijini Warsaw.


"Niliwaona wao katika mechi ya kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Ukraine Ijumaa). Katika kipindi cha kwanza walicheza vvizuri sana, wakiwa na nafasi nyingi za kufunga mabao,” alisema Hodgson.


"Kama wao watacheza vizuri kesho Jumanne (leo) dhidi yetu, kama walivyocheza kipindi cha kwanza dhidi ya Ukraine, basi mechi yetu itakuwa ngumu.


"Lakini daima mimi nimekuwa nikiwaunga mkono wachezaji. Nawaamini wao, hasa ukizingatia sisi ndio pekee ambao hatujafungwa mechi katika kundi letu.


"Tuna uwezo wa kuendeleza kutofungwa kwetu katiika mechi ya 10, na ukizingatia tutakuwa na nafasi ya kupewa sapoti na mashabiki wetu tutakapocheza Wembley, nitawasapoti wao. Nitakuwa mjinga kutowapa nguvu nyota wangu," alisisitiza Hodgson.


RATIBA YA MECHI ZA LEO KOMBE LA DUNIA - BARANI ULAYA

Cyprus             v          Albania           

Ugiriki              v          Liechtenstein                           

Lithuania           v          Bosnia-Herzegovina     

Azerbaijan        v          Russia             

Israel                v          Ireland Kask.             

Ureno               v          Luxembourg               

Norway            v          Iceland            

Uswisi              v          Slovenia                     

Hungary           v          Andorra                     

Romania           v          Estonia                       

Uturuki v          Uholanzi                      

Latvia               v          Slovakia                                 

Bulgaria            v          Jamh. Czech               

Denmark          v          Malta                         

Serbia              v          Macedonia                 

Jamh. Ireland    v          Kazakhstan                

Sweden            v          Ujerumani        

Vis. Faroe        v          Austria            

Italia                 v          Armenia                     

Ufaransa           v          Finland

Hispania           v          Georgia           

San Marino      v          Ukraine                      

Montenegro      v          Moldova                    

England            v          Poland             

Ubelgiji v          Wales                         

Scotland           v          Croatia            


BBC/Supersport.com

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments