Michuano vilabu bingwa Ulaya kuendelea

Unknown | 2:26 PM | 0 comments

Harry Kane

Mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane ataendelea kuuguza jeraha lake la kifundo cha mguu wakati ambapo timu yake inakabiliana na CSKA Moscow katika kombe la vilabu bingwa Ulaya siku ya Jumanne.

Tottenham itamkosa beki wake wa kushoto Danny Rose na kiungo wa kati Eric Dier,Mousa Dembele na Moussa Sissoko.

Katika mechi nyengine itakayohusisha klabu ya Uingereza,kipa wa Leicester Kasper Schmeichel huenda akarudi kuichezea klabu yake katika mchuano wa kwanza wa kombe la vilabu bingwa Ulaya kwa klabu hiyo kushiriki nyumbani wakati watakapoikaribisha klabu ya Ureno Porto.

Schmeichel amekuwa nje kwa mechi tatu tangu Leicester iishinde Cub Brugge katika mechi yao ya ufunguzi ya Kundi G.

Mechi nyengine zitakazochezwa hii leo ni:
CSK vs Tottenham
Leicester vs FC Porto
Monaco vs Bayer Levkn
Bor Dortmd vs Real Madrid
Sporting vs Legia War
FC Copenhagen vs Club Brugge
Dinamo Zagreb vs Juventus
Sevilla vs Lyon

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments