Hii ndio Top 6 ya mastaa wa soka wenye hasira zaidi uwanjani
Moja kati ya michezo inayoongoza kwa
kuchukua headlines duniani ni mchezo wa soka ambao nchi nyingi ndio
mchezo wanaoupa kipaumbele kuliko michezo mingine, huu ni mchezo ambao
una headlines ya rekodi kibao ila leo November 28 naomba nikusogezee Top 6 ya wachezaji wa soka wanaotajwa kuwa na hasira zaidi.
6- Diego Costa ni mkali wa soka anayekipiga katika klabu ya Chelsea ya Uingereza
ila ni moja kati ya wachezaji wenye hasira zaidi uwanjani hususani pale
inapotokea kachezewa faulo kwa bahati mbaya na mchezaji wa timu pinzani
basi huwa hayaishi kirahisi uwanjani.
5- Zlatan Ibrahimoic ni staa wa soka kutokea Sweden lakini anakipiga katika klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa ana
headlines kadhaa ila ya ukorofi na kubishana na refa hiyo pia ni moja
kati ya sifa zake, huwa anatajwa kupaniki pale anapochezewa faulo.
4- Gennaro Gattuso alikuwa anakipiga katika klabu ya AC Milan na baadae Sion
ila ana headlines kadhaa za kuoneshwa kadi kutokana na utamaduni wake
wa kujibizana na marefa pale ambapo anapokuwa anapingana na maamuzi yao
uwanjani haoni hasari kumfokea refa au mchezaji wa timu pinzani pale tu
anapokuwa hajaridhdishwa na tukio fulani.
3- Roy Keane huyu ni kiungo wa zamani wa klabu ya Manchester United ya Uingereza
ambaye amewahi kutamba sana kwa umahiri wake katika nafasi ya kiungo,
ukitaja wachezaji wenye hasira katika soka hakika huyu huwezi kumkosa,
kwa sasa amestaafu soka.
2- Oliver Khan ni golikipa wa Ujerumani amecheza timu ya taifa na amewahi kuitumikia klabu ya FC Bayern Munich lakini ni moja kati ya magolikipa bora waliowahi kuitumikia Bayern na Ujerumani. yupo nafasi ya pili katika list ya wachezaji wenye hasira uwanjani.
1- Pepe ni beki wa kimataifa wa Ureno anayeichezea klabu ya Real Madrid ya Hispania,
ukorofi na matukio yake anayofanya uwanjani yamefanya kuwa anaoneshwa
kadi nyekundu mara kwa mara uwanjani, sio aina ya mchezaji ambaye
atavumilia jambo lisilomfurahisha lipite lakini ni mchezaji anayependa
kufanya faulo za makusudi uwanjani.
Category: uingereza
0 comments