NGOMA DROO KATI YA TAIFA STARS NA TIMU YA MSUMBIJI "MAMBAZ"

Unknown | 9:57 PM | 0 comments


TIMU ya Taifa ya Tanzania, 'Taifa Stars' imetoshana nguvu na timu ya Taifa ya Msumbiji 'Mambaz' katika mechi ya kufuzu Kombe la Mataifa Afrika 2015 kwa sare ya mabao 2-2.
Mechi hiyo iliyokuwa na upinzani mkubwa imepigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Stars yote mawili yamewekwa kimiani na Khamis Mcha dakika ya 65 na 71 kwa mkwaju wa penalti huku ya Mambaz yakifungwa na Elias Pelembe kwa penalti dakika ya 47 na Isac Carvalho dakika ya 87.

Share story hii kupitia>>>>>> :
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Category:

0 comments